Jumanne, 5 Novemba 2013

Mkenya, Lupita Nyong’o atwaa tuzo ya Hollywood

Image

Muigizaji wa Kenya, Lupita Nyong’o ametwaa tuzo yake ya kwanza ya Hollywood Film Awards zilizofanyika huko Beverly Hilton jijini Los Angeles, Marekani.
Image

Lupita Nyong’o akitoa shukrani
Nyong’o ameshinda tuzo New Hollywood Award kwa kuigiza filamu ya ’12 Years A Slave’ iliyoanza kuoneshwa kwenye majumba ya sinema Marekani na Uingereza wikiendi iliyopita.

Pamoja na hivyo, Nyong’o amekuwa akitajwa miongoni mwa waigizaji wanaoweza kuwania kipengele muigizaji bora msaidizi wa kike kwenye tuzo Oscar.
Image

Lupita alijikuta akibubujikwa na machozi ya furaha wakati akitoa maneno yake ya shukrani

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni